DKT. ULIMBOKA ASIMULIA TUKIO
Akisumulia tukio hilo 
Dkt Ulimboka alisema kuwa jana usiku alipigiwa simu
 na mtu aliyejitambulusha kwake kuwa anaitwa Hemed
, aliyemwambia kuwa anahitaji kuongea naye,
na ndipo
 walipopanga kuonana katika eneo la
 Leaders Kinondoni.
Dk Ulimboka aliyekuwa akiongea kwa tabu, aliendelea 
kusimulia kuwa wakati akiongea na mtu huyo anayekiri
 kuwa alikuwa akifahamiana naye kabla, alikuwa na
 wasiwasi kwani kila mara alikuwa akipokea simu na
 kuwasiliana na watu wengine ambao hawakuwapo 
eneo hilo.
Alisema baada ya muda alishangaa kuona
 wanaongezeka
 watu wengine watano wakiwa na silaha, kisha
 wakamwambia kuwa anahitajika kituo cha Polisi na
 kumvuta
 na kumuangusha barabarani kabla ya kumuingiza katika
 gari lenye rangi nyeusi na kuondoka naye.
Dkt Ulimboka alisema kuwa wakiwa njiani walimpiga,
 na kumfikisha katika msitu huo wa 
pande na kuendelea kumpiga paka alipoteza fahamu.
MADAKTARI SASA KUMWEKEA ULINZI
Lakini, uchunguzi  umebaini kuwa wodini alikolazwa Dk Ulimboka, kuna ulinzi mkali wa madaktari na hairuhusiwi watu kumwona kiholela siyo tu kwa sababu za kutaka aachwe apumzike, bali pia kutowaamini watu ovyo.
Madaktari wanaolinda eneo hilo walisikika jana wakisema, “Huyu tunamlinda wenyewe na haiwezekani mtu asiyefahamika kuingia humu ndani, na hilo tutahakikisha sisi wenyewe,”alisikika akisema mmoja wa madaktari hao.
Kiongozi jopo la madaktari
Katika hatua nyingine, kiongozi wa jopo la madaktari wanaomuhudumia Dk Ulimboka, Profesa Joseph Kahamba aliwaambia waandishi wa habari kuwa Dk Ulimboka ana majeraha mwili mzima.
“Ingawa kwa sasa anaendelea vizuri, Dk Ulimboka ameumia sana, kwani mwili wake mzima una majeraha kutokana na kupigwa na watekaji hao,”alisema Profesa Kahamba na kuongeza:
“Aliumia mbavuni,kifuani, miguuni, mikononi ambako aling’olewa baadhi ya kucha za vidole na kichwani na kinywani, ambako aling’olewa meno mawili,”alisema.
Alifafanua kwamba, kutokana na maumivu hayo ya kichwa, Dk Ulimboka alipata tatizo la mtikisiko wa ubongo, lakini akasisitiza kuwa madaktari bingwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha yake.
Madaktari wanaolinda eneo hilo walisikika jana wakisema, “Huyu tunamlinda wenyewe na haiwezekani mtu asiyefahamika kuingia humu ndani, na hilo tutahakikisha sisi wenyewe,”alisikika akisema mmoja wa madaktari hao.
Kiongozi jopo la madaktari
Katika hatua nyingine, kiongozi wa jopo la madaktari wanaomuhudumia Dk Ulimboka, Profesa Joseph Kahamba aliwaambia waandishi wa habari kuwa Dk Ulimboka ana majeraha mwili mzima.
“Ingawa kwa sasa anaendelea vizuri, Dk Ulimboka ameumia sana, kwani mwili wake mzima una majeraha kutokana na kupigwa na watekaji hao,”alisema Profesa Kahamba na kuongeza:
“Aliumia mbavuni,kifuani, miguuni, mikononi ambako aling’olewa baadhi ya kucha za vidole na kichwani na kinywani, ambako aling’olewa meno mawili,”alisema.
Alifafanua kwamba, kutokana na maumivu hayo ya kichwa, Dk Ulimboka alipata tatizo la mtikisiko wa ubongo, lakini akasisitiza kuwa madaktari bingwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha yake.
Vyanzo:TZMPAKAAU,Solo Thang,Globalpublishers na Mtwara Kumekucha 
 
No comments:
Post a Comment