Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Wednesday, November 7, 2012

BENI KINYAIYA AHAMIA CLOUDS TV



“Heeey Fun’z  I am officially announce kwamba now nimehamia  CLOUDS TV so usikose kunicheki kwenye kipindi  change kuanzia  Jumamosi hii saa 8:05pm uone zile FUJO zangu Luningani kama kawa Leee Gooo “ BENI KINYAIYA SUVEREEEEE.

KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA ZAIDI WA MAUAJI YA BARLOW HATIMAYE RADIO CALL, FUNGUO ZA GARI ALILOKUWA NALO MAREHEMU VYAPATIKANA

NA ALBERT G. SENGO: MWANZA

Radio call (simu ya upepo) iliyokuwa ikitumiwa na aliyekuwa kamanda wa jeshi la polisi Mwanza marehemu Liberatus Barlow hatimaye imenaswa  ikiwa imefichwa kwenye shimo la maji taka (septic tank) kwenye moja ya nyumba eneo la Nyashana jijini Mwanza.

Kunaswa kwa Radio call hiyo kumekuja kufuatia kukamatwa kwa watu wengine watatu zaidi wakituhumiwa kuhusika na mauaji hayo.

Watu hao waliokamatwa mara baada ya kutajwa na washirika wenzao watano ambao tayari wako mahabusu ni pamoja na Abdalah Petro Ndayi (32) mkazi wa Mjimwema jijini Mwanza, Abdalahman Ismail (28) mkazi wa Mkudi Ghana, na Lyoba Matiku anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 46-50 akiwa ni mkazi wa Nyakabungo jijini Mwanza huyu anatajwa kuwa ndiye mfadhili wa kundi hilo la ujambazi na mipango yote ya uvamizi hufanyika kwake. 



Msikilize kwa kubofya play Mkuu wa kitengo cha upelelezi wa makosa ya Jinai wa Jeshi la polisi mkoani Mwanza, Joseph Konyo  anafafanua zaidi... 


Vielelezo vingine vilivyokamatwa nyumbani kwa mtuhumiwa Abdalah Petro Ndayi ni pamoja na Ufunguo mmoja wa gari alilokuwa akiendesha Kamanda Liberatus Barlow siku ya tukio, sim card za mitandao mbalimbali, simu nne za mkononi kila moja ikiwa na laini yake, kofia mbili aina ya barreti kati ya hizo moja ni ya polisi na nyingine ni ya kampuni ya ulinzi.

Vielelezo vingine ni sare moja (suruali na shati) ya rangi ya blue yenye mstari mweupe ya moja ya makampuni ya ulinzi jijini Mwanza,  suruali moja ya kaki inayofanana na sare za mgambo wa jiji la Mwanza ikiwa na masalia ya damu kwenye pindo la suruali kwa nyuma, kipande cha nondo, bisibisi na sare inayotumiwa na askari wa polisi kikosi cha kutuliza ghasia FFU...
 
PICHA NA HABARI ZA TUKIO NI KW AHISANI YA ALBAT G SENGO WA MWANZA

BENDI YA MSONDO KUZINDUA VYOMBO VIPYA LIDAZ CLUB IJUMAA

BENDI Kongwe ya mziki wa dansi nchini Tanzania Msondo Music inatarajia kuzindua vyombo vyake vipya kabisa walivyokabidhiwa hivi karibuni na Kampuni ya KONYAGI akizungumza na waandishi wa habari msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema tumeshapewa vyombo na Konyagi ambavyo tutavizindua mbele ya mashabiki wetu siku ya Ijumaa pale LIDAZ CLUB siku ya Ijumaa hivyo wapenzi wote wa bendi ya Msondo mnaombwa kuhudhuria kwa wingi ili kuona vyombo vipya
Pamoja na kupata burudani za bendi hiyo zikiwemo nyimbo za zamani na za sasa kwa ajili ya kuanza wik end Super D aliongeza kwa kusema wapenzi watakaokuja siku hiyo watapata burudani za radha tofauti tofauti kwani wamepanga kukonga nyoyo za mashabiki wao kwa kutumia vyombo vyao vipya 
Bendi hiyo siku ya Jumapili itamaliza burudani za wik end katika ukumbi wa Max Bar Ilala bungoni

Mkurugenzi wa Bendi hiyo Muhidini Maalimu Gulumo ataongoza kundi zima la wana msondo ngoma akiwemo Said Mabera, Shabani Dede, Romani Mn'gande, Eddo Sanga, Juma Katundu, Hassani Moshi na wendine kibao kwa ajili ya kuwaburudisha mashabiki.

ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI LA SHINYANGA AFARIKI DUNIA‏

 Kifo cha askofu ALOYSIUS BALINA wa jimbo katoliki la shinyanga kilichotokea leo siku ya jumanne majira ya saa tano za asubuhi katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando mkoani Mwanza alikokuwa amelazwa kwa matibabu na kimethibitishwa pia na Mkurugenzi wa habari wa jimbo kuu la Mwanza padre CHRISTOPHER KUBEJA pamoja na tanzia ya jopo la mapadri washauri wa jimbo la shinyanga.




Padri KUBEJA amesema kuwa mipango ya mazishi inafanyika jimboni shinyanga na kuwataka waumini wa kanisa hilo kuwa watulivu... Msikilize kwa kubofya Play


TANZIA 
JOPO LA WASHAURI WA ASKOFU JIMBO KATOLIKI SHINYANGA KWA NIABA YA MAPADRE, WATAWA, WALEI NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA.
WANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MHASHAMU ASKOFU ALOISIUS BALINA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA KILICHOTOKEA LEO TARAHE 6 NOVEMBER 2012 SAA 5:00 ASUBUHI KATIKA HOSPITALI YA RUFAA BUGANDO.
HABARI ZIWAFIKIE MAASKOFU, MAPADRE, WATAWA NA WAUMINI WOTE POPOTE WALIPO.
MIPANGO YA MAZISHI INAANDALIWA JIMBONI SHINYANGA.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.
IMETOLEWA NA 
MKURUGENZI WA HABARI 
JIMBO KUU LA MWANZA 
PADRE CHRISTOPHER KUBEJA

Mhe. Selasini wa CHADEMA na Mhe. Mrema wa TLP wamfagilia Rais Kikwete kwa uchapaji kazi‏

OBAMA ASHINDA KUIONGOZA MAREKANI KWA MIAKA 4


Ni miaka minne mingine kwa rais Barack Obama. Rais huyo wa kwanza mweusi kuliongoza taifa kubwa zaidi duniani ametangazwa asubuhi ya leo kuwa mshindi katika mchuano mkali na wa aina yake.
Ilikuwa ni kama ndoto iliyozimika katika makao makuu ya kampeni ya Mitt Romney mjini  Alabama wakati matokeo yakianza kumiminika hasa kutoka katika majimbo yenye maamuzi ambayo yote yalikuwa yanaelekea kwa rais Obama. Wakati kimya kikitanda katika  kambi ya Romney na wafuasi wake wakionekana kutoamini kilichotokea, jimboni Chicagohali ilikuwa ya nderemo na vifijo.
Wafuasi wa chama cha Democrats wakishangalia wakati matokeo yakiendelea kutolewa. Wafuasi wa chama cha Democrats wakishangalia wakati matokeo yakiendelea kutolewa.
Mitt Romney ameshinda kura ya umma kwa asilimia 50 lakini mfumo wa Marekani unazingatia kura za majimbo kupata mshindi. Obama ameshinda licha ya rekodi mbaya ya uchumi na ukosefu mkubwa wa ajira. Hakuna raia aliyewahi kupata muhula wa pili tangu kumalizika kwa vita vikuu vya pili vya dunia, kukiwa na ukosefu wa ajira wa zaidi ya asilimia 7.2. Kiwango cha sasa ni asilimia 7.9.
Matokeo yalianza  kwa kutangazwa ushindi wa  Rais Obama  katika jimbo la Vermont, yakifuatia majimbo ya Delaware, Maryland, Michigan, Pennyslivania, Wisconsin na New Hampshire . Kwa na  mpinzani wake Mitt Romney alinyakua ushindi wa  mikoa inayofahamika kuegemea upande wa chama chake cha Republican, ikiwa ni pamoja na  Kentucky, Tennese, South Carolina, West Virginia na  Indiana.

Tuesday, November 6, 2012

NAVUTIWA SANA NA UVAAJI HUU JAMANI DAH

NA SIKUZOTE INA WAPENDEZA SANA MA BINTI WA KIAFRIKA KUVAA VAZI HILI NIGERIA NI MIONGONI MWA NCHI AMBAZO KATIKA HAFLA YEOYOTE BASI KINA MAMA AU WAREMBO HUJISITIRI KWA VAZI HILI  AMBAPO HUWA INANIVUTIA SANA NA HAKIKA HALICHOKI WALA KUCHUJA.




Uchaguzi waanza Marekani

Wapiga kura nchini Marekani wameanza zoezi la kumchagua rais atakaeiongoza nchi yao kwa miaka minne ijayo. Hadi siku ya mwisho ya kampeni, kura za maoni ziliwaonyesha wagombea wawili wa wadhifa huo, Rais Barack Obama na mpinzani wake wa chama cha Republican Mitt Romney wakiwa nguvu sawa, ingawa Obama anaonekana kuongoza kwa kiwango kidogo. 


Akitoa rai ya mwisho kwa wapiga kura, Mitt Romney alisema mlango uko wazi kwa ushindi.

Rais Obama alitoa rai sawa na hiyo kwa wanaomuunga mkono jimboni Ohio. Kwa upande mwengine Warepublican wamelalmika juu ya kimbunga kilichoikumba Marekani wiki iliyompita kwamba kumepunguza kasi ya mgombea wao.

Monday, November 5, 2012

Arusha Artists na track "Arusha Kilele"

 
Katika kusherehekea Arusha kuwa Jiji,Artists kutoka kaskazini kwa pamoja wamerecord track pande za noizmekah studios kwa hisani kuu ya Serikali yaani ofisi ya mkuu wa mkoa na Manispaa ya jiji na nyimbo inakwenda kwa jina la "Arusha Kilele" inayozungumzia mema na mazuri tele kuhusu Arusha.sikiliza na kudownload hapa kusupport Tanzanian music.

CHECK OUT:AFTER PARTY YA FETTY BAADA YA KUGRADUATE

                                                 Ilikua ni party flani ya kiaina tu, kusherehekea kumaliza kwa miaka yangu mitatu ya kutafuta na kufanikiwa kuipata elimu ya chuo kikuu. shukrani zote nazipeleka kwa Mungu kwa kuendelea kuniazima pumzi yake na kunielekeza vyema.
                              Pichani ni Washikaji wakipata msosi wa nguvu                       
 Nikki wa pili kwa mbaali namuona Dina Marios
  Antu Mandoza akipata msosi wa nguvu kabisa

My good friend's Uncle Shaa and his friend Calvin
                                                                        B Twelve na Faraja
                                                                          Shilole
                                                                     Warembo    
                                                                       Ncha kali
                                                                        Darasa
                                                                       B Dozen
 Muli B
                                                                          Sofia
                                                                       Darasa
                                                                        B dozen
                                                  Thats ma girl Shade

                                            Kulia,Faraja na kushoto kwangu ni Millard Ayo
                                                                     
                                                                          Nikki wa pili
Issa Wendo hahahaaaaa hatari sana huyu kaka
                                                                                  Jaffarai 
Ticha shiiipu hahahaaaa mshkaji wangu, kaka yangu, ndugu yangu, chizi mwenzangu thats him Evarist
Mgomvi wangu dunia nzima Tannisa aka Real tanny....
Mtu wa watu Chibebi
                                                                             Ncha kali
                                                                        Soudy Brown
                                                                    Cute couple Issa and Nurie
                                                               Muna mindu weeeeeee,  Burudani mwanzo mwisho
                                                       DeeAndy,Soudy Brown,Ncha kali 
                                                                       Tumetokelezea
kwa hisani ya dj fetty blog

MISS TANZANIA 2012-2013

 Brigette Alfred kutokea Kanda ya Kinondoni (Sinza).Akiwa amewabwaga wenzake 29 waliokuwa wakiwania taji hilo.Na kujipatia zawadi yake ya Gari aina ya Noah na pesa taslim Tsh ml 8.Hongera sanaaaaa!!

SERIKALI KUTOA DAWA ZA KUTIBU KISUKARI BURE KWA WATANZANIA WENYE TATIZO HILO.

Serikali imetangaza kutoa bure dawa za kutibu ugonjwa wa kisukari ili kuokoa maisha ya watanzania wanaokabiliwa na ugonjwa huo kutokana na kuwepo kwa ongezeko la wagonjwa wa kisukari kwa siku za karibuni.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii SEIF RASHID amesema hatua hiyo ya Serikali imefikiwa kutokana na kupatikana kwa gharama kubwa kwa dawa za ugonjwa wa kisukari na kuwa watu wanaokabiliwa na ugonjwa huo wanapaswa kutumia dawa hizo kwa maisha yao yote huku idadi kubwa wakiwa ni watoto.

Kauli hiyo ya Serikali imekuja kufuatia swali la Mbunge wa Viti Maalum SUSAN LYIMO ambaye ameiomba Serikali kutoa bure dawa za ugonjwa wa kisukari kama ilivyo kwa dawa za kutibu magonjwa mengine sugu ikiwemo UKIMWI

Saturday, November 3, 2012

WEEKEND NJEMA NAKUACHA NA MAPISHI YA NYAMA YA NGOMBE NA MAHARAGWE

Mapishi ya nyama ya ng'ombe na maharagwe
Mahitaji Maharagwe gramu 350, nyama ya ng'ombe gramu 150, chumvi gramu 5, chembechembe za kukoleza ladha gramu 8, sukari gramu 5, pilipili hoho gramu 5, vipande vya vitunguu maji gramu 3, mchuzi wa sosi gramu 3. Njia 1. kata nyama iwe vipande, koroga nyama pamoja na wanga. 2. washa moto, mimina maji kwenye sufuria, baada ya kuchemka, tia maharagwe kwenye maji, korogakoroga, yapakue. Tia mafuta kwenye sufuria, halafu tia vipande vya nyama kwenye sufuria, korogakoroga vipakue. 3. washa moto tena, tia pilipili hoho korogakoroga, halafu tia maharagwe korogakoroga, halafu tia vipande vya nyama, tia chumvi, chembechembe za kukoleza ladha, mchuzi wa sosi, korogakoroga, tia sukari korogakoroga, halafu mimina maji ya wanga korogakoroga, ipakue, mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Rais Kikwete azindua rasmi Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela - Arusha (NM-AIST)‏

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi  Hati ya Ardhi ya eneo la   Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali ambaye ndiye Mkuu wa Chuo hicho katika sherehe za uzinduzi wake rasmi  Ijumaa Novemba 2, 2012. Kulia ni Makamu Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Burton Mwamila.




 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi toka kwa Makamu Mkuu wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Profesa Burton Mwamila  jijini Arusha. Kushoto ni  Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali ambaye ndiye Mkuu wa Chuo hicho katika sherehe za uzinduzi wake rasmi  Ijumaa Novemba 2, 2012.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012. 

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua sanamu ya Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini Mzee Nelson Mandela  wakati wa uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe  wakati wa uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012. Pamoja naye ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali ambaye ndiye Mkuu wa Chuo hicho, WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Burton Mwamila, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Magessa Mulugo, 


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela. Kulia ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali ambaye ndiye Mkuu wa Chuo hicho katika sherehe za uzinduzi wake rasmi  Ijumaa Novemba 2, 2012.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya utafiti wa dawa asilia toka kwa Meneja Mauzo wa kampuni ya madawa asilia ya Moringa Natural Products Bi. Christina Ngoty wakati wa  uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya utafiti wa mitishamba toka Dkt Efrem Akilei Njau wakati wa  uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Arumeru Mashariki Mhe Joshua Nassari wakati   uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu wa zamani Mzee Edwin Mtei  wakati   uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.
Wageni waalikwa wakimshamgilia Rais Kikwete baada ya kuzindua rasmi  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha za pamoja wakati wa  uzinduzi rasmi wa  Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela  jijini Arusha  Ijumaa Novemba 2, 2012.