Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, June 5, 2014

HAYA KAZI KWENU WAPENDA KUONYESHA MIILI YENU HADHARANI INSTAGRAM YAFUTA PICHA ZA UCHI



Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ameambia BBC kuwa sheria zake kuhusu picha za uchi hazimbagui mtu yeyote.
Kampuni hiyo imekosolewa vikali kwa kwa kuondoa picha za wanawake walio nusu uchi kwenye mtandao huo.

Lakini Afisaa mkuu mtendaji wa mtandao huo wa kijamii, Kevin Systrom, amesema kuwa sheria hizo zinalenga kuhakikisha kuwa vijana na watu wazima wanaotumia mtandao huo wako salama.
Masharti ya matumizi ya mtandao wenyewe, yanasema: 'Mtu haruhusiwi kuweka picha za watu walio nusu uchi na picha zenye mada ya ngono. ''
Matamshi yake yanakuja baada ya mwanawe muigizaji maarufu, Bruce Willis, Scout Willis kuweka picha yake kwenye mtandao huo akiwa nusu uchi bila kitu kifuani.
Picha hiyo iliondolewa kwenye mtandao huo na wamiliki wa mtandao na hapo ndipo malalamiko yalianza kuibuka.

Muimbaji Rihanna, ambaye alikuwa na wafuasi milioni 1.3 aliunga mkono kampeini hiyo kabla ya kufunga akaunti yake.

Wamiliki wa mtandao huo wanasema sheria zinapaswa kufuatwa na kila mtu awe mtu mashuhuri au vinginevyo.

"lengo letu ni kuhakikisha kuwa Instagram, ni mahala salama kwa kila mtu , awe maarufu au la. ''
"tunapaswa kuwa na sheria na kuhakikisha kuwa kila mtu anafuata sheria hizo. Bila shaka tunapata changamoto nyingi lakini tutnaedneklea kusisitiza umuhimu wa sheria kufuatwa, '' alisema Systrom
Huku umaarufu wa mtandao huo ukiendelea kuimarika, mtandao huo umekosolewa kuhusiana na baadhi ya picha zinazochapishwa humo . Pia mtandao wenye umebana baadhi ya maneno yanayohusiana na madawa ya kulevya.
Instagram ilinunuliwa na Facebook mwaka 2012.

Chanzo cha habari BBC swahili.

No comments:

Post a Comment