Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, May 28, 2015

MWANAMUZIKI MWENYE ASILI YA TANZANIA NA ITALIA SHANTEL SAROLDI ASEMA MUZIKI WA TZ UNANAFASI KUBWA

Mwanamuziki mwenye asili ya Tanzania  na Italia  CHANTAL SAROLDI amesema  muziki wa Tanzania unayo nafasi kubwa kimataifa kutokana na Watu kutoka nje kupendelea sana nyimbo zenyeasili ya nchi za Kiafrika.






Mwanamuziki huyo amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na maonesho atakayoifanya jijini kwa  mualiko wa ubalozi wa Itali nchini.

Amesema muziki wa wanamuziki kutoka Afrika ikiwemo Tanzania wanapaswa kufanyaziara za mara kwa mara nje ya nchi zao ili kuutangaza muziki wao huku akithibitisha kua Raiya wa Italia wanapenda sana utamaduni hasa wa nyimbo kutoka barani Afrika.

Nae balozi wa ITALI nchini Tanzania LUIGI SCOTTO amesma muziki ni moja ya njia za kukuza ushirikiano hivyo ubalozi wake umeamua kumualika mwanamuziki huyo ambaye mamayake ni raiya wa Tanzania huku babayake akiwa muitalia ili kuja kuonesha jinsi Tanzania na Italii zilivyokuwa na urafiki wa karibu.

Kuhusiana na ziara ya mwanamuziki huyo , msimamizi wa maonesho hayo SAMANTAR ABDINUR LUSUF amesema ziara ya mwanamuziki huyo itamfikisha pia katika kisiwa cha Zanzibar.

UEFA YAITAKA FIFA KUHAIRISHA UCHAGUZI WA VIONGOZI.

Baada ya jana kushuhudia baadhi ya maofisa wa FIFA wakitiwa nguvuni kwa kile kinachodaia kujihusisha na rushwa katika michuano ya kombe la dunia,Shrikisho la soka Barani Ulaya UEFA limeitaka FIFA kuhairisha uchaguzi wa Shirikisho hilo kwa siku ya kesho kutokana na kashfa iliyotokea hapo jana.

MAADHIMISHO SIKU YA HEDHI DUNIANI



Mnyama Simba akikosa nyama wakati mwingine hulazimika kula hata nyasi ilimradi tu adhibiti njaa inayomkabili na maisha yaende.

Ndivyo ilivyo kwa Wasichana na akimama wengi maeneo ya Vijijini ambao hulazimika kutumia kanga na vitenge kama mbadala wa Taulo Maalum za kike maarufu kama pedi.

Changamoto ya ukosefu wa taulo maalum za kike inatajwa kuhatarisha Afya za Wasichana na Wanawake wengi Vijijini kutokana na kutumia vifaa ambavyo si salama kwa afya zao pindi wanapoingia kwenye hedhi.
 
Meneja Mradi uliojikita kuwasaidia Wanafunzi wa Kike Mashuleni kutoka Shirika la Maendeleo la Uholanzi, (SNV), ROZALIA MUSHI, anatumia Siku ya hedhi Duniani kufafanua zaidi ukubwa wa tatizo hilo katika maeneo ya Vijijini.

Kila anaetoa chozi anasababu inayopelekea chozi hilo kulazimika kumtoka, Wakati Wasichana wa Vijijini wakikumbwa na tatizo la ukosefu wa taulo za kike na kulazimika kutumia njia mbadala, wale wa maeneo ya Mijini na wao wana kilio chao.
                                                                                              
Kila jambo lina chanzo chake na hapa ROZALIA MUSHI anabainisha kilichochangia Dunia kulazimika kuiadhimisha Siku hii.

Camera na kipaza sauti cha Clouds Tv hakikuishia hapo kinaelekezwa katika moja ya maduka yanayofanya biashara ya Mataulo maalum ya kike ili kubaini hali ya biashara hiyo na upatikanaji wake.

Lakini je hali ya miundombinu kwenye Shule mbalimbali nchini pindi Mwanafunzi anapoingia kwenye Siku zake akiwa yupo maeneo ya Shule ipoje..? MADINA KEMILEMBE ni Afisa Elimu Mkuu, Kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anaeleza azidi.


Siku ya hedhi Duniani imeambatana na kauli mbiu isemayo “ Usisite kuzungumzia hedhi’’ kauli hii inatokana na kitendo cha Wanajamii wengi kuhofia kuzungumzia Siku hiyo.

SHULE YA MSINGI LIWITI NA MSEWE ZAKABILIWA NA UKOSEFU WA CHOO.



Na JAMES LYATUU
 Zaidi ya wanafunzi 2,000 wa shele za msingi  LIWITI na MSEWE zilizopo Tabata Liwiti  manispaa ya Ilala Jijini Dar es salam wako hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kufuatia kukosekana kwa huduma ya choo shuleni hapo.

Blog hii imefika hadi shuleni hapo nakujionea wanafunzi wakijisaidia katika vichaka, nyumba za majirani, misikitini na Bar jambo linaloweza kuhatarisha usalama na afya zao kama halitopatiwa ufumbuzi mapema.
Wakizungumza na kituo hiki baadhi ya wanafunzi wa shule hizo wameeleza kuwa hali hiyo imekuwa ikiwapa wakati mgumu pindi wanapopatwa na aja kubwa au ndogo jambo linalowafanya kushindwa kusoma kwa ufanisi.

Nao majirani ambao wamekuwa wakiwasaidia wanafunzi hao kwenda kujisaidia katika vyoo vyao wameeleza kuwa hali hiyo imekuwa usumbufu mkubwa kwao huku wakionyesha hofu ya wanafunzi hao kubakwa kutokana na kuingia kila nyumba kwenda kuomba huduma ya choo.

James Lyatuu  amezungumza na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa eneo hilo WILFRED MSHANA ambapoa anakiri kuwepo kwa tatizo hilo katika kata yake huku akitupia lawama uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ilala kwa kushindwa kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.

Lakini pia anaeleza kuwa hivi karibuni watoto wawili wa shule hizo waliangukia chooni kisha wakanusurika baada ya kutolewa na walimu wa shule hiyo kwa kushirikiana na wananchi.

 
Jitiada za kuzungumza na uongozi wa shule zote hizo mbili hazikufanikiwa baada ya viongozi wa shule hizo kutotoa ushirikiano wowote kwa kituo hiki huku wakieleza kuwa mkurugenzi wa manispaa ya Ilala ndio msemaji.

Juhudi za kumpata mkurugenzi wa manispaa ya Ilala ilikutolea ufafanuzi suala hilo hazikuzaa matunda.

FERRE GOLLA MIONGONI MWA WANAMUZIKI AMBAO NAWAKUBALI SANA



 Mfahamu kwa jina la ferre gola shelani ni miongoni mwa vijana ambao nawakubali sana kutokana na utendaji kazi wao kwanza amejaliwa sauti na anakipaji cha hali ya juu hebu fuatilia hizi nyimbo zake mbili halafu nitakuambia zaidi sikunyingine kwanini nasema hayo wakati huo na wewe nakupa ruhsa ya kumtafakari halafu nambie.
kwakuanza hapa anakuambia  Eyindaka Mabe fuatilia angalia alivyocheza na sauti ni shidah Ferré Gola .

haya hapa anakuja na kitu kingine anakuambia Pakadjuma hii ni moja ya nyimbo ambazo nazihusudu sana.


haya na wewe funguka nambie unaonaje.... mie Muziki wa afrika upo katika damu ni vigumu kuusahau ukweli hujitenga siku zote unagana na mie hapa kama kuna unayokosa kuhusu muziki huo niulize nitakujibu kwenye blog ndani

WAZEE WAONDOKANA NA TATIZO LA UKOSEFU WA VYOO

Mmoja wa wazee wanaoishi kwenye kambi hiyo Simon Maganga amesema hayo wakati wakikabidhi choo, na magodoro kutoka asasi ya eazy flex amesema kuwa hapo awali walikuwa wanalazimika kujisaidia vichakani kutokana na choo kuwa mbali na makazi yao .

 Mratibu wa asasi ya Eazy Flex Hapines kihampa amesema kuwa msaada waliotoa kwenye kituo hicho unagharimu zaidi ya million 20 ukiwemo ujenzi wa choo, ununuzi wa viti na madogoro kwa ajili ya kuwapunguzia wazee hao adha ya kulala chini.

Makabidhiano hayo yaliudhuliwa na meya wa manispaa ya shinyanga Gulam Hafidhi ambapo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum na si kuziachia asasi za kiraia.
Kituo cha kolandoto kina jumla ya wazee 60 ambao wanaishi kwenye kambi hiyo huku wakikabiliwa na changamoto ya makazi na kulazimika kuishi kwenye nyumba mbovu.

Wednesday, May 27, 2015

KAMA ULIIKOSA HII HAPA EXCLUSIVE: MAHOJIANI NA EDWARD LOWASSA 02



EXCLUSIVE MAHOJIANO YA EDWARD LOWASSA 2015 KAMA ULIYAKOSA HAYA HAPA MAHOJIANO NA EDWARD LOWASSA NO 01



TUJIKUMBUSHE KOFFI OLOMIDE ALIPOTEMBELEA TANZANIA NA KUFANYA MAHOJIANO NA CLOUDS FM


TUKO PAMOJA BADO

Hakika nafsi ya mtu hubeba mambo mengi sana na siri NZITO mmno laiti tungeweza kuyaona yalio katika nafsi za wenzetu sijui ingekuwaje, lakini mwenyezi MUNGU anajua sababu ya kutokuwezesha binadamu kuona kwa macho yetu, yalio katika nafsi za wenzetu unaweza tabasamu lakini kilichomondani ya nafsi yako unakijua wewe na MUNGU wako namshukuru MUNGU kwamba niko mzima, mwenye furaha kila wakati and am verry strong, verry strong. #sinamaana yeoyote natafakari tu....