Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, March 12, 2015

WATOTO, VIJANA, WATU WAZIMA NA HATA WAZEE WAKO HATARINI KUKUMBWA NA TATIZO LA FIGO



Ni wakati wa jioni wanaonekana Vijana zaidi ya Watano wakisikiliza Redio, mara linasikika tangazo linalohamasisha upimaji wa afya zao, wote wanapuuza na mmoja wao anabadilisha kabisa stesheni na kutafuta nyingine.


Baada ya wiki kupita mmoja wa Vijana hao ghafla hali ya mwili wake inaanza kubadilika anahisi uchovu muda wote, na miguu yake kuvimba hivyo wanalazimika kumkimbiza hospitali.

Kutokana na kutojenga utamaduni wa kupima afya zao, mara baada ya vipimo anabainika kuwa na tatizo la figo lakini kibaya zaidi Daktari anawajuza kuwa tatizo la rafiki yao ni kubwa zaidi kutokana na kuchelewa kubainika.
Hali hiyo ndiyo inayoelezwa kuwakumba Wagonjwa wengi wanapelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbi… 

Tatizo la figo linaelezwa kuendelea kuwa kubwa nchini ambapo kwa wiki katika Hospitali hiyo pekee wanapokea wagonjwa kuanzia 8 hadi 10.
Watoto, Vijana, watu wazima na hata Wazee wako hatarini kukumbwa na tatizo hilo.

Kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), idadi ya vifo vitokanavyo na magonjwa ya figo nchini imefikia 4533 sawa na asilimia1.03  ya vifo vyote, wakati kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa figo kimeripotiwa kuwa asilimia 14 .

No comments:

Post a Comment