Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, July 5, 2012

Ecobank Kuendelea Kuikopesha NHC Ijenge Nyumba

BENKI ya Ecobank imeahidi kuendelea kulikopesha zaidi Shirika la Nyumba la Taifa  (NHC), katika mradi wa kujenga nyumba na kukopesha ili kuhakikisha Watanzania  wengi wanapata nyumba bora na za bei nafuu.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu.
Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, James  Cantamantu-Koomson, ametoa ahadi hiyo wakati baada ya hafla  iliyoandaliwa na NHC kwa ajili ya kutiliana saini mkataba wa mkopo na taasisi  tisa za fedha juzi jijini Dar es Salaam.
Katika hafla hiyo, Ecobank ilisaini kutoa mkopo wa Sh bilioni 2.1 na imeahidi  kuwa itaongeza kiasi kingine cha fedha siku zijazo ili kufanikisha mradi huo  wenye manufaa kwa wananchi.
Mkurugenzi huyo alisema Ecobank inawajali Watanzania na imeahidi kuunga mkono  kwa dhati mpango huo wa NHC ili kuwakomboa Watanzania wengi ambao hawana makazi  bora kutokana na kipato kidogo.
“Sisi Ecobank mradi kama huu si mgeni kwetu, tunajali na kuthamini sana  masuala ya makazi, karibu nchi zote 30 tunazofanya kazi zetu tunashiriki miradi  kama hii, kuwapa wananchi nyumba bora ni jambo la muhimu sana,” alisema.
Ndugu Cantamantu-Koomson alisema ingawa benki hiyo ina miaka miwili tu tangu ianze kutoa huduma zake  nchini, imejitahidi kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya Watanzania na kushiriki  katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Mwishoni mwa mwaka 2011, NHC ilipewa kibali na Serikali kukopa kwenye taasisi  za fedha za ndani na nje ya nchi ili kuendeleza miradi ya ujenzi
Kwa ujumla Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limesaini mikataba ya mkopo wa Sh bilioni 165 kutoka kwa taasisi nyinginezo  tisa za fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa miradi ya ujenzi wa nyumba pamoja na ununuzi wa ardhi ya akiba.
Taasisi za fedha zilizotoa  mkopo huo pamoja na kiwango walichotoa kwenye mabano ni pamoja na CRDB (Sh bilioni 35), ECO Bank (Sh bilioni 2.1), TIB (Sh bilioni 22), BancABC  (Sh bilioni 4.2), NMB (Sh bilioni 26), CBA (Sh bilioni 24), LAPF (Sh bilioni  15), Azania (Sh bilioni saba) na Shelter Afrique (Sh bilioni 23).

SOURCE http://monfinance.com/ FOR MORE INFORMATION

No comments:

Post a Comment