Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Wednesday, January 18, 2012

MBUNGE WA CCM JEREMIA SUMARI WA JIMBO LA ARUMERU AFARIKI DUNIA "


TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa, mbunge wa Jimbo la Arumeru kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Jeremia Sumari amefariki dunia leo.

Mbunge huyo alikuwa akisumbuliwa na maradhi kwa kipindi kirefu na wakati anakutwa na mauti leo alfajiri alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.


Jeremia Sumari ni mbunge wa pili kwa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kufariki kwa mwaka huu 2012 baada ya kutanguliwa na mbunge wa viti maalum Chadema, Regia Mtema.

MWENYEZI MUNGU AMALAZE MAHALI PEMA PEPONI
 AMIN.

No comments:

Post a Comment