Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, May 28, 2015

MAADHIMISHO SIKU YA HEDHI DUNIANI



Mnyama Simba akikosa nyama wakati mwingine hulazimika kula hata nyasi ilimradi tu adhibiti njaa inayomkabili na maisha yaende.

Ndivyo ilivyo kwa Wasichana na akimama wengi maeneo ya Vijijini ambao hulazimika kutumia kanga na vitenge kama mbadala wa Taulo Maalum za kike maarufu kama pedi.

Changamoto ya ukosefu wa taulo maalum za kike inatajwa kuhatarisha Afya za Wasichana na Wanawake wengi Vijijini kutokana na kutumia vifaa ambavyo si salama kwa afya zao pindi wanapoingia kwenye hedhi.
 
Meneja Mradi uliojikita kuwasaidia Wanafunzi wa Kike Mashuleni kutoka Shirika la Maendeleo la Uholanzi, (SNV), ROZALIA MUSHI, anatumia Siku ya hedhi Duniani kufafanua zaidi ukubwa wa tatizo hilo katika maeneo ya Vijijini.

Kila anaetoa chozi anasababu inayopelekea chozi hilo kulazimika kumtoka, Wakati Wasichana wa Vijijini wakikumbwa na tatizo la ukosefu wa taulo za kike na kulazimika kutumia njia mbadala, wale wa maeneo ya Mijini na wao wana kilio chao.
                                                                                              
Kila jambo lina chanzo chake na hapa ROZALIA MUSHI anabainisha kilichochangia Dunia kulazimika kuiadhimisha Siku hii.

Camera na kipaza sauti cha Clouds Tv hakikuishia hapo kinaelekezwa katika moja ya maduka yanayofanya biashara ya Mataulo maalum ya kike ili kubaini hali ya biashara hiyo na upatikanaji wake.

Lakini je hali ya miundombinu kwenye Shule mbalimbali nchini pindi Mwanafunzi anapoingia kwenye Siku zake akiwa yupo maeneo ya Shule ipoje..? MADINA KEMILEMBE ni Afisa Elimu Mkuu, Kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anaeleza azidi.


Siku ya hedhi Duniani imeambatana na kauli mbiu isemayo “ Usisite kuzungumzia hedhi’’ kauli hii inatokana na kitendo cha Wanajamii wengi kuhofia kuzungumzia Siku hiyo.

No comments:

Post a Comment