Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Thursday, May 28, 2015

SHULE YA MSINGI LIWITI NA MSEWE ZAKABILIWA NA UKOSEFU WA CHOO.



Na JAMES LYATUU
 Zaidi ya wanafunzi 2,000 wa shele za msingi  LIWITI na MSEWE zilizopo Tabata Liwiti  manispaa ya Ilala Jijini Dar es salam wako hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kufuatia kukosekana kwa huduma ya choo shuleni hapo.

Blog hii imefika hadi shuleni hapo nakujionea wanafunzi wakijisaidia katika vichaka, nyumba za majirani, misikitini na Bar jambo linaloweza kuhatarisha usalama na afya zao kama halitopatiwa ufumbuzi mapema.
Wakizungumza na kituo hiki baadhi ya wanafunzi wa shule hizo wameeleza kuwa hali hiyo imekuwa ikiwapa wakati mgumu pindi wanapopatwa na aja kubwa au ndogo jambo linalowafanya kushindwa kusoma kwa ufanisi.

Nao majirani ambao wamekuwa wakiwasaidia wanafunzi hao kwenda kujisaidia katika vyoo vyao wameeleza kuwa hali hiyo imekuwa usumbufu mkubwa kwao huku wakionyesha hofu ya wanafunzi hao kubakwa kutokana na kuingia kila nyumba kwenda kuomba huduma ya choo.

James Lyatuu  amezungumza na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa eneo hilo WILFRED MSHANA ambapoa anakiri kuwepo kwa tatizo hilo katika kata yake huku akitupia lawama uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ilala kwa kushindwa kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.

Lakini pia anaeleza kuwa hivi karibuni watoto wawili wa shule hizo waliangukia chooni kisha wakanusurika baada ya kutolewa na walimu wa shule hiyo kwa kushirikiana na wananchi.

 
Jitiada za kuzungumza na uongozi wa shule zote hizo mbili hazikufanikiwa baada ya viongozi wa shule hizo kutotoa ushirikiano wowote kwa kituo hiki huku wakieleza kuwa mkurugenzi wa manispaa ya Ilala ndio msemaji.

Juhudi za kumpata mkurugenzi wa manispaa ya Ilala ilikutolea ufafanuzi suala hilo hazikuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment