Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Sunday, November 11, 2012

CCM yamrudisha tena kwenye medani za siasa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho JAPHET PHILLIP MANGULA

 
 
Hatimaye Chama Cha Mapinduzi CCM kimemrudisha tena kwenye medani za siasa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho  JAPHET PHILLIP MANGULA baada Kamati Kuu ya Chama hicho iliyoketi jana Mjini Dodoma kupitisha jina lake kugombea nafasi ya Makamu wa Mwenyekiti CCM Taifa Bara.
 
Kwa uteuzi huo  MANGULA sasa ataungana na Rais JAKAYA KIKWETE ambaye amepitishwa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho taifa huku Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK ALLI MOHAMED SHEIN akipitishwa kuwa makamu Mwenyekiti Zanzibar.
 
Akizungumza Mjini Dodoma Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi amesema, chama chake kimeamua kumrudisha MANGULA ili kukiongezea nguvu huku ikirejea dhana yake ya kuwafikia wakulima na wafanyakazi.


Katika hatua nyingine NAPE ametangaza mabadiliko ya ratiba ambapo kwa sasa uchaguzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa viti kumi bara na viti kumi Zanzibar utafanyika leo na mkutano
kutarajiwa kumalizika Novemba 13 mwaka huu.



No comments:

Post a Comment