Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Wednesday, June 3, 2015

CCBRT YATOA MATIBABU BURE KWA MATIBABU YA WATOTO WENYE NYAYO ZILIZOPINDA.



Tatizo la kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu bado limeendelea kuwepo katika jamii, kama ambavyo imetokea kwa NAOMI JACOB aliejifungua mtoto mwenye nyayo zilizopinda na kujikuta akibezwa na jamii kutokana na tatizo hilo.


  
Kufuatia kadhia hiyo, Naomi alijiona kama hana thamani katika jamii,  hali ambayo kwa sasa imepata ufumbuzi baada ya Hospitali ya CCBRT ya jijini Dar es salaam kuanza kutoa matibabu ya bure, kwa watoto waliozaliwa na tatizo la nyayo zilizopinda kama anavyoeleza.


DKT. GETRUDE JOSEPH ni daktari wa idara ya mifupa kutoka hospitali ya CCBRT, ambae ameeleza kuwa tatizo hilo limekuwa likiongezeka kila kukicha, kwa kutopewa kipaumbele na jamii.

Nae GASPER NJELUAH ambae ni daktari wa idara ya mifupa kutoka hospitali ya Temeke, ameeleza chanzo nyayo zilizopinda, huku akiiasa jamii kutowatenga watoto wenye tatizo hilo.

Kwa mujibu wa takwimu zilizofanywa na shirika la Ponsetti zimeeleza kuwa, takribani watu laki mbili huzaliwa na tatizo la nyayo zilizopinda ulimwenguni kila mwaka, ambapo asilimia 80 kati yao wanatokea nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.










No comments:

Post a Comment