Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, June 22, 2015

WANANCHI HAWANAUELEWA WA FURSA ZILIZOKO NDANI YA JUMUIYA YA EAC



Wakati ushuru wa forodha ukiondolewa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki hali inayowawezesha Wananchi kutoka nchi hizo wanachama kufaidika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika Jumuiya hiyo bado Watanzania wengi hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na fursa hizo.

Baadhi ya Wakazi Jijini Dar es salaam akiwemo CHINDO YAHAYA na ALEX NZALI ambao wamekiri kutokuwa na uelewa kuhusiana na fursa zinazopatikana katika Jumuiya hiyo.

Na hizi ni baadhi ya fursa zinazopatikana ndani ya Jumuiya hiyo kama anavyobainisha Mchumi Kutoka Wizara ya Afrika Mashariki, AMEDEUS MZEE.

Wakati baadhi ya nchi ndani ya Jumuiya hiyo zikija na mpango wa kutumia vitambulisho kuvuka mipaka ya nchi hizo kwa kutumia usafiri wa aina mbalimbali msimamo wa Tanzania ni upi huyu hapa AMEDEUZI anafafanua.

Katika kuhakikisha utengamano wa Afrika Mashariki unaimarika zaidi vilianzishwa Vyombo mbalimbali ikiwemo Mahakama inayosimamia kesi zote katika eneo hilo ambayo ipo mjini Arusha, Tanzania na Bunge la Afrika Mashariki lenye Wajumbe wajumbe 27 ambao wanachaguliwa na mabunge ya nchi wanachama.

No comments:

Post a Comment