Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, June 22, 2015

YOGA DAY- JE UNAFAHAMU FAIDA ZA YOGA NA YOGA YENYEWE SOMA ZAIDI HAPA



Watu wengi leo hufikiria sana jinsi wanavyoweza kuwa na mwili mwembamba na afya nzuri, Jambo hilo limefanya wengi watafute msaada katika klabu za mazoezi ya viungo vya mwili na pia za kuboresha afya.
 Kwa sababu hiyo hiyo, maelfu ya watu kutoka nchi za Magharibi wamegeukia yoga mfumo wa mazoezi ulioanzishwa miaka zaidi ya mia 5 iliyopita katika nchi za Mashariki huku chimbuko lake likiwa nchini India.


Yoga ni mfumo wa mazoezi ya maungo na kudhibiti pumzi,  Watu wanaokabiliana na msongo wa mawazo, mshtuko wa moyo, na mfadhaiko pia wamegeukia yoga ili kupata faraja na utatuzi wa matatizo yao. 

Kutafakari kama kule kunakofanywa na Dini ya Uhindu ambako kulitokana na yoga, kumependwa sana kwa sababu wacheza-sinema na wanamuziki wa roki wanapenda aina hiyo ya yoga.

Godfrey Malik  ni mstaafu ambaye alianza kufanya mazoezi ya yoga zaidi ya miaka 15 iliyopita hapa anakiri kupata unafuu wa maisha tangu aanze mazoezi hayo.

Inadaiwa kwamba mazoezi ya yoga ni tiba ya magonjwa mbali mbali yasiyoambukizwa, na kumekuwepo na unafuu mkubwa kwa watu wanaotumia aina hiyo ya mazoezi huku nchini watu wengi zaidi wameitokeza kushiriki na kujifunza aina hiyo ya mazoezi kama anavyoeleza balozi mdogo wa india nchini.

Ili utamaduni huo uwezi kuingia katika jamii yetu ya kitanzania, kuna umuhimu wa kuwashirikisha wanafunzi katika mazoezi hayo ili waweze kujifunza wakiwa watoto, kama wahenga walivyowahi kusema, “samaki mkunje angali mbishi”.
 
Je, kuna ukweli wowote kuhusu mazoezi hayo ya yoga kuchangia katika kudhibiti au kuponya magonjwa mbali mbali ya binadamu?,  tumekutana na daktari Rajni Kanabar ambaye anaeleza kwa kifupi faida za mazoezi ya yoga.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kwamba Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeamua kuadhimisha siku ya kimataifa ya yoga, Juni 21, kwani ni aina ya mazoezi au masomo ambayo maadili yake ni sambamba na yale ya Umoja wa Mataifa.

Katika taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Ki-moon amenukuliwa akisema kwamba mazoezi hayo yanayochezwa tangu enzi za kale yana manufaa kwa afya ya mwili na akili ya binadamu.


Watu wengi leo hufikiria sana jinsi wanavyoweza kuwa na mwili mwembamba na afya nzuri, Jambo hilo limefanya wengi watafute msaada katika klabu za mazoezi ya viungo vya mwili na pia za kuboresha afya.


Kwa sababu hiyo hiyo, maelfu ya watu kutoka nchi za Magharibi wamegeukia yoga mfumo wa mazoezi ulioanzishwa miaka zaidi ya mia 5 iliyopita katika nchi za Mashariki huku chimbuko lake likiwa nchini India.

Yoga ni mfumo wa mazoezi ya maungo na kudhibiti pumzi,  Watu wanaokabiliana na msongo wa mawazo, mshtuko wa moyo, na mfadhaiko pia wamegeukia yoga ili kupata faraja na utatuzi wa matatizo yao. 

Kutafakari kama kule kunakofanywa na Dini ya Uhindu ambako kulitokana na yoga, kumependwa sana kwa sababu wacheza-sinema na wanamuziki wa roki wanapenda aina hiyo ya yoga.

Godfrey Malik  ni mstaafu ambaye alianza kufanya mazoezi ya yoga zaidi ya miaka 15 iliyopita hapa anakiri kupata unafuu wa maisha tangu aanze mazoezi hayo.

Inadaiwa kwamba mazoezi ya yoga ni tiba ya magonjwa mbali mbali yasiyoambukizwa, na kumekuwepo na unafuu mkubwa kwa watu wanaotumia aina hiyo ya mazoezi huku nchini watu wengi zaidi wameitokeza kushiriki na kujifunza aina hiyo ya mazoezi kama anavyoeleza balozi mdogo wa india nchini.

Ili utamaduni huo uwezi kuingia katika jamii yetu ya kitanzania, kuna umuhimu wa kuwashirikisha wanafunzi katika mazoezi hayo ili waweze kujifunza wakiwa watoto, kama wahenga walivyowahi kusema, “samaki mkunje angali mbishi”.

Je, kuna ukweli wowote kuhusu mazoezi hayo ya yoga kuchangia katika kudhibiti au kuponya magonjwa mbali mbali ya binadamu?,  tumekutana na daktari Rajni Kanabar ambaye anaeleza kwa kifupi faida za mazoezi ya yoga.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kwamba Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeamua kuadhimisha siku ya kimataifa ya yoga, Juni 21, kwani ni aina ya mazoezi au masomo ambayo maadili yake ni sambamba na yale ya Umoja wa Mataifa.

Katika taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Ki-moon amenukuliwa akisema kwamba mazoezi hayo yanayochezwa tangu enzi za kale yana manufaa kwa afya ya mwili na akili ya binadamu.

No comments:

Post a Comment