Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, June 15, 2015

MUFTI MKUU WA TANZANIA SHEIKH SHAABAN SIMBA AFARIKI DUNIA.

Na JAMES LYATUU 
Habari zilizotufikia hivi punde zinaarifu kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Shaaban Issa Simba amefariki dunia.

Akidhibitisha kutokea kwa kifo hicho Shehe Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Mussa Salim amesema Mufti amefikwa na umauti hii leo asubuhi katika Hospitali ya TMJ alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

"Ni kweli Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Shaaban Issa Simba amefariki hii leo asubuhi kwa maradhi ya sukari na presha," alisema kwa ufupi Sheikh Alhhadi.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo na unataraji kusafirishwa kesho kwenda  mkoani Shinyanga  kwaajili ya maziko. 
Father Kidevu Blog inaungana na waislamu wote nchini katika maombolezo na inawapa pole Familia yake, ndugu jamaa na marafiki na wailsamu wote ndani na nje ya Tanzania. 
INNA LILLAH WA INNA ILLAHI RAJIUN.


No comments:

Post a Comment