Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, October 27, 2014

AUSTRALIA YAZUIYA WATU WANAOTOKA MATAIFA YALIOKUMBWA NA MLIPUKO WA EBOLA KUINGIA NCHINI HUMO




Australia imezuia kwa muda pasi za kusafiria kwa watu wanaotaka kuingia nchini mwao hasa wale wanaotoka nchi za Afrika Magharibi  nchi ambazo zimekumbwa na mlipuko wa ebola.

lengo la Australia ni kujaribu kuzuia virusi visiweze kutoka na kusambaa nakuingia katika  mipaka yake.

Waziri wa uhamiaji , Scott Morrison, ameliambia bunge mapema leo  Jumatatu kwamba serikali yake imeamua kusimamisha kwa muda utoaji wa  viza kwa watu kutoka nchi hizo zilizoadhiriwa na  ugonjwa huo, ambao umepoteza maisha ya watu wengi tangu kuzuka kwake. Huku  zaidi ya kesi  10,000 zikiripotiwa katika nchi hizo.

No comments:

Post a Comment