Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, October 27, 2014

UCHAGUZI WA BRAZIL DILMA ROUSSEFF AAHIDI MAGEUZI BAADA YA KUSHINDA UCHAGUZI.




Rais Dilma Rousseff ameahidi kuiunganisha nchi ya Brazil baada ya kushinda kwa kuchaguliwa tena kwa awamu ya pili kwa asilimia 51.6% ya kura. 



Licha ya upinzani  wa karibu nusu  ya wapiga kura nchini Brazil , rais Dilma Rousseff hatimae amechaguliwa  tena kwa mhula wa pili wa kipindi kingine cha miaka minne, ukiwa pia ushindi wa nne wa chama chake cha wafanyakazi.


Bibi Rousseff mwenye umri wa miaka 69 na ambaye wakati wa ujana wake alikuwa mpiganaji wa chini kwa chini mfuasi wa nadharia ya Marx amemshinda mpinzani wake Aecio Neves  kutoka chama cha Social Democrats  kwa asili mia 51 dhidi ya 49 ya kura.



Bi Rousseff, ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2010, bado maarufu Brazil kwa programu ya ustawi wa serikali yake,a
nakabiliwa na changamoto ya kuyatatua matatizo ya kiuchumi, huduma  mbaya za umma na rushwa.


No comments:

Post a Comment