Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

Bondia wa TZ kuzipiga Afghanistan


Hamid Rahimi atatoana jasho na mtanzania Said Mbelwa.

Afghanistan inaandaa pigano la kwanza la ndondi kuwahi kufanyika nchini humo huku kukiwa na ulinzi mkali sana.

Masumbwi hayo yanayohusisha wanamasumbwi wa uzani wa middle, yenye kauli mbiu ya ''kupigania amani'' yatapeperushwa moja kwa moja kupitia televisheni.

Mamilioni ya waafghanistan wanatarajiwa kutizama mchuano huo kati ya bingwa wa ndondi nchini Afghanistan, Hamid Rahimi, na mshindani wake kutoka Tanzania, Said Mbelwa.
Ndondi ziliharamishwa nchini Afghanistan mwishoni mwa utawala wa Taliban.

kwa hisani ya BBC swahili.

No comments:

Post a Comment