Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Monday, October 29, 2012

MKUU WA WILAYA YA KIBAHA AKEMEA VIJANA JUU YA MAKUNDI‏

MKUU wa Wilaya ya kibaha,mkoani Pwani Halima Kihemba amekemea tabia ya vijana ambao wanajiingiza katika makundi ya kihuni ambayo hayana tija yoyote na  yanaweza kusababisha uvunjifu wa amani kutokana na kujichukulia sheria mikononi.

Kihemba amekemea hali hiyo wakati alipokuwa akizungumza na  na viongozi na vijana wa Wilaya ya kibaha ambao wanatarajiwa kuanza kujiandaa kwa ajili ya kuanza  mafunzo ya ujasilimali,ambapo amesema anachukizwa sana na  vijana wenye jazba ambao wamekuwa wakivamia hata vituo vya polisi na kureta vurugu.

Pia Kihemba pia ametoa wito kwa wazee wa Wilaya ya kibaha kuhakikisha kwamba wanaisaidia serikali yao  katika kuwaelimisha vijaa kuachana na mwenendo wa kujiingiza katika makundi mabaya yamekuwa ni moja ya chanzo cha kuleta mogogoro.

NA MWANDISHI VICTOR KUTOKA KIBAHA.

No comments:

Post a Comment