Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Wednesday, October 31, 2012

JINSI YA KUPIKA NYAMA YA BATA NA BIA

Mahitaji: Nyama ya bata gramu 500, pilipili hoho gramu 5, tangawizi gramu 10, vitunguu saumu gramu 5, bia chupa moja, chumvi gramu 8, sukari gramu 6, mchuzi wa sosi gramu 10, mafuta gramu 70, pilipili manga gramu 5, wanga gramu 5.   Njia ya kupika: 1. osha nyama ya bata, halafu uikate iwe vipande vipande, kata tangawizi na vitunguu saumu viwe vipande. 2. washa moto, halafu tia mafuta kwenye sufuria tia nyama ya bata, korogakoroga halafu tia vipande vya tangawizi, vitunguu maji, korogakoroga, halafu mimina bia na supu, baada ya kuchemka, tia chumvi, sukari na mvinyo wa kupikia na kupunguza moto, endelea kuchemsha kwa dakika 30, tia pilipili hoho na pilipili manga, halafu mimina maji ya wanga korogakoroga, na ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

No comments:

Post a Comment