Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

Wakimbizi wa Burundi nchini TZ warejeshwa makwao

 

Serikali ya Tanzania imeanza rasmi hatua za kuwarejesha makwao raia wa Burundi waliovuliwa hadhi ya ukimbizi.

Ni katika hatua za kuifunga rasmi kambi ya Mtabila ambayo ni kambi pekee iliyokuwa ikihifadhi wakimbizi wa Burundi nchini humo wapatao elfu thelathini na saba.
Shughuli ya kuwarejesha makwao kwa hiyari raia wa Burundi waliokuwa wakimbizi hadi mwezi Agosti mwaka huu kabla ya kuvuliwa hadhi ya ukimbizi na serikali ya Tanzania,ilimalizika rasmi Jumatatu ambapo kuanzia leo kinachofuata dhidi ya wakimbizi hao ni kuandikishwa kwa kufuatwa kwenye maeneo wanakoishi kambini na kisha kupakiwa kwenye magari na kurejeshwa Burundi.
Akizungumza na mwandishi wa BBC mjini Dar es Salam Eric David Nampesya, mkuu wa kambi hiyo ambaye ni mwakilishi wa wizara ya Mambo ya ndani nchini humo, Bwana Frederick Nisajile, alisema utaratibu huo utakavyokuwa baada ya kukamilika kwa shughuli ya kurejea kwa hiyari ya 'Kimombo Voluntary repatriarition.'
Bwana Nisajile alisema inatarajiwa kuwa raia wa Burundi wapatao elfu moja watarejeshwa makwao kila siku katika utaratibu huu ambao pia utawahusisha maafisa wa idara ya Uhamiaji ili kuwakamata wale wote watakaokaidi kurejea makwao.

kwa hisani ya BBC swahili.

No comments:

Post a Comment