Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

Zuma na Motlanthe wakosoana hadharani

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini na makamu wake Kgalema Motlanthe wamekosoana hadharani mbele ya wanahabari jambo lililoonyesha kuwepo vita vya kung'ang'ania madaraka ndani ya chama tawala nchini humo ANC.

Mapema Makamu wa Rais wa Afrika Kusini alikuwa amesema kwamba nchi iko katika hali ngumu na kwamba uchumi umesimama.

 Baadaye Rais Zuma amejitokeza mbele ya vyombo vya habari na kusema matamshi ya makamu wake hayaakisi ukweli wa mambo kwani uchumi unasonga mbele na unakua kila siku.

 Hii ni katika hali ambayo viongozi hao wanatarajiwa kuchuana kwenye uchaguzi wa chama baadaye mwaka huu.

 Montlanthe amesema chama cha ANC kinahitaji mabadiliko kwani uongozi wa sasa umepoteza dira na kwa kiwango kikubwa umeitumbukiza nchi pabaya.

Rais Zuma amekasirishwa na matamshi hayo na kusisitiza kuwa huo si msimamo rasmi wa serikali.

No comments:

Post a Comment