Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

MKUU wa Mkoa wa Tanga Luten Mstaaf Chiku Galawa amezindua mashindano ya kitaifa ya michezo ya Kitaifa ya mpira wa kikapu

MKUU wa Mkoa wa Tanga Luten Mstaaf Chiku Galawa amezindua mashindano ya kitaifa ya michezo ya Kitaifa ya mpira wa kikapu ambapo pamoja na mambo mengine amewakata wananchi kuudhamini mchezo huo kama ilivyo katika mchezo wa soka.
Akizungumza na wanamichezo hao kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini pamoja na Mambo mengine mkuu huyo wa Mkoa amewaasa wanamichezo kuwachagua viongozi wa michezo wenye uwezo wa kuimarisha mchezo huo na ambao hawatafanyakazi kwa maslahi yao binafsi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na timu zilizoshiriki katika mashindano hayo Katibu Mkuu wa Mpira wa Kikapu Alexernder Msoffe amesema timu nyingi zimeshindwa kushiriki katika michuano hiyo kutokana na tatizo la uhaba wa fedha.
Michuano hiyo itachukua muda wa juma moja na timu 22 kutoka mikoa 11 hapa nchini zimeshiriki.

No comments:

Post a Comment