Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

Mbinu mpya ya bei nafuu kupima HIV



Ikiwa mtu anavirusi rangu ya kifaa inabadilika kuwa buluu na ikiwa hana rangi unakuwa nyekundu
Aina mpya mbinu ya kuchunguza na kuona hata viwango vya chini vya virusi na hata aina ya saratani imezinduliwa na watafiti nchini Uingereza.
Utafiti huo unahusu majimaji ambayo hubadilika rangi kuonyesha ikiwa mtu ameathirika au la.
Aidha watafiti wansema mbinu hii mpya ambayo inahitaji utafiti zaidi, inaweza kuelezea kwa kina aina ya ugonjwa au virusi mfano proteni inayopatikana kwenye kirusi cha HIV.
Ikiwa dalili ya kirusi au ugonjwa ipo katika matokeo ya uchunguzi, basi inabadili rangi ya kemikali. Matokeo yatakuwa rangi ya buluu ikiwa kirusi kipo na nyekundu ikiwa kirusi au ugonjwa haupo.
Watafiti wanasema kuwa matokeo ya uchunguzu au upimaji pia yatapatikana mara moja.
Profesa Molly Stevens aliambia BBC: " Mbinu hii ya kupima magonjwa inatumiwa kuchunguzwa virusi hata kama ni vya viwango vya chini mno na kuongeza nafasi ya kuona ikiwa ugonjwa upo kwenye mwili wa mtu au la.

Hiki ni kifaa ambacho mtu anaweza kujipima mwenyewe hali yake ya HIV akiwa nyumbani
"Kwa mfano, ni muhimu kuchunguza viini vya ugonjwa vilivyo na viwango vya chini sana vya mfano saratani kwa mtu aliwahi kutibiwa ugonjwa huo kuona ikiwa saratani hiyo itaweza kuibuka tena hata baada ya kutibiwa."
"pia inaweza kusaidia katika kupima wagonjwa wa HIV, ambao viwango vya virusi viko chini sana kiasi cha kutoweza kuonekana kwa mbinu za sasa."
Watu waliopimwa mapema kutumia mbinu hii ya rangi, walionyesha dalili za HIV na saratani ya tezi ya kibofu, ingawa utafiti wake katika nyanja za juu bado utahitajika kabla ya kutumika hospitalini.
Watafiti wanasema kuwa wanatarajia kuwa gharama ya kifaa hicho itakuwa ndogo mara kumi kuliko mbinu za sasa za kupima magonjwa na kwamba itanufaisha watu katika nchi ambazo mbinu zilizopo hawawezi kuzimudu. Na pia itaweza kutumika sana katika kupima virusi vya HIV katika nchi maskini duniani.

No comments:

Post a Comment