Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tuesday, October 30, 2012

Kimbunga cha Sandy chazidisha maafa USA

Kimbunga kikali mno cha Sandy kilichoanza kuikumba miji mbalimbali muhimu ya Marekani kinaendelea kusababisha maafa makubwa nchini humo.

 Zaidi ya watu milioni 6.5 hawana huduma za umeme katika majimbo ya pwani ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Watu wasiopungua 12 wameaga dunia hadi sasa kutokana na kimbunga hicho kikali. Upepo mkali na mvua kubwa zinazonyesha sambamba na kimbunga hicho zinatabiriwa kuathiri maeneo mengi ya kaskazini mashariki mwa Marekani.

 Kimbunga cha Sandy kimesababisha pia hasara ya mabilioni ya dola nchini humo. Vituo vingi vya treni vimejaa maji, maelfu ya safari za ndege zimevunjwa, mamia ya maelfu ya watu wameondolewa katika maeneo mbalimbali ili kueupusha maafa na matatizo mengine mengi.

No comments:

Post a Comment