Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Tunapatikana Sinza kwa Remmy

Friday, April 6, 2012

RAIS BINGU WA MUDHARIKA AFARIKI DUNIA.



Mwanzoni redio ya taifa ilikuwa imetangaza kwamba Mutharika, mwenye miaka 78, angelipelekwa Afrika Kusini kwa matibbabu zaidi, lakini inaonekana kwamba alishafariki dunia wakati alipofikishwa hospitali.
Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo, Makamu wa Rais Joyce Banda, ndiye anayechukuwa nafasi ya kiongozi wa nchi, ingawa kuondolewa kwa Banda kutoka chama tawala hapo mwaka 2010 kunaweza kutatiza kipindi cha mpito.
Mutharika, aliyewahi kufanya kazi kama mchumi kwenye Benki ya Dunia, amekuwa akituhumiwa kwa kushindwa kuongoza na kutokuuendeleza uchumi wa nchi hiyo. Inasemekana alikuwa akimtayarisha mdogo wake, Waziri wa Mambo ya Nje Peter wa Mutharika, kuwa mrithi wake. Mara kadhaa, Peter amekuwa akionekana akikaimu wadhifa wa kaka yake anapokuwa hayupo.

Maandamano ya mwaka 2011 dhidi ya Mutharika mjini Lilongwe. Maandamano ya mwaka 2011 dhidi ya Mutharika mjini Lilongwe.
Polisi katika mji mkuu, Lilongwe wameimarisha usalama, tangu tangazo la maradhi ya ghafla ya Mutharika ilipotangazwa hapo jana, huku wanajeshi wakionekana karibu na nyumba ya Banda.

No comments:

Post a Comment